Na MASHIRIKA
MCHUANO wa mkondo wa pili katika hatua ya 32-bora ya Europa League kati ya Arsenal na Benfica ya Ureno sasa utachezewa jijini Athens, Ugiriki.
Mechi hiyo imepangwa kusakatwa mnamo Februari 25 uwanjani Georgios Karaiskakis ambao hutumiwa na Olympiakos kwa minajili ya mechi zao za nyumbani.
Mechi hiyo iliyokuwa iandaliwe uwanjani Emirates ilihamishwa hadi Ugiriki baada ya serikali ya Uingereza kupiga marufuku safari za watu wanaoingia Uingereza kutoka baadhi ya mataifa, ikiwemo Ureno.
Masharti hayo mapya yanapania kuzuia msambao wa maambukizi mapya ya virusi vya corona.
Mchuano wa mkondo wa kwanza wa kipute hicho ulihamishwa hadi uwanjani Olimpico, Roma na utatandazwa mnamo Februari 18.
Mchuano wa mkondo wa kwanza wa hatua ya 32-bora kwenye Europa League kati ya Manchester United na Real Sociedad ya Uhispania utachezewa jijini Turin, Italia mnamo Februari 18 huku marudiano yakiandaliwa ugani Old Trafford, Uingereza wiki moja baadaye.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO