• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:55 AM
Nusu-fainali ya kukata na shoka

Nusu-fainali ya kukata na shoka

LONDON, Uingereza

Na MASHIRIKA

Arsenal itavaana na Liverpool nayo Chelsea ifufue uhasama dhidi ya Tottenham katika nusu-fainali za kudondosha mate za Carabao Cup mnamo Januari 3-10.

Wanabunduki wa Arsenal walimiminia Sunderland mabao 5-1 katika nusu-fainali Jumanne. Liverpool walitoka chini 3-1 na kubandua Leicester kwa njia ya penalti 5-4 Jumatano. Muda wa kawaida ulimalizika 3-3 baada ya Leicester kutinga mabao kutoka kwa Jamie Vardy (mawili) na James Maddison nao Alex Oxlade-Chamberlain, Diogo Jota na Takumi Minamo kufungia Liverpool.

Kocha Mikel Arteta atakosa huduma za Mghana Thomas Partey, Mgabon Pierre-Emerick Aubameyang na Mmisri Mohamed Elneny naye kocha Jurgen Klopp hatakuwa na washambuliaji Mohamed Salah (Misri), Naby Keita (Guinea) na Sadio Mane (Senegal) wakati wa nusu-fainali za Carabao.

Wachezaji hao wanaelekea kwenye Kombe la Afrika (AFCON) nchini Cameroon.Arsenal ilizamisha Sunderland kutoka ligi ya daraja ya tatu kupitia magoli ya Eddie Nketiah (hat-trick yake ya kwanza kabisa), Nicolas Pepe na kinda Charlie Patino.Vijana wa Arteta watakuwa wakitafuta kufika fainali ya Carabao kwa mara ya kwanza tangu 2018 walipopoteza dhidi ya Manchester City.

Watalimana na Wolves na City ligini kabla ya Carabao. Liverpool, ambayo inafukuzana vilivyo na City kwenye vita vya kuwania taji la Ligi Kuu, itapepetana na Leicester na Chelsea ligini kabla ya kukutana na Arsenal.Chelsea ya kocha Thomas Tuchel ilikanyaga Brentford 2-0 kupitia magoli ya kuchelewa kutoka kwa Jansson (alijifunga) na Jorgino (penalti).

Tottenham ya kocha Antonio Conte ilitamba ugani Tottenham dhidi ya West Ham kupitia magoli ya Steven Bergwijn na Lucas Moura. Jarrod Bowen alipachika bao la West Ham.

You can share this post!

Azma ya Shujaa ni kujiinua Dubai 7s

Timu ya voliboli ya ufukweni ilivyong’ara hadi...

T L