• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 3:55 PM
Real Madrid wakomoa Osasuna na kuendelea kuifuata Barcelona kwenye mbio za kusaka taji la La Liga

Real Madrid wakomoa Osasuna na kuendelea kuifuata Barcelona kwenye mbio za kusaka taji la La Liga

Na MASHIRIKA

REAL Madrid wanaendelea kuifuatwa Barcelona baada ya kukomoa Osasuna 2-0 ugenini katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumamosi.

Real walikosa huduma za mfumaji Karim Benzema kwenye safu ya mbele katika mchuano huo ulioshuhudia wakifungiwa mabao na Federico Valverde na Marco Asensio.

Mabingwa hao watetezi wa La Liga walipoteza nafasi za kufunga mabao zaidi kupitia kwa Vinicius Jr. Alvaro Rodriguez na David Alaba nao walimtatiza pakubwa kipa Sergio Herrera wa Osasuna.

Baada ya mechi za Jumapili, Real sasa wanakamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali la La Liga kwa alama 51 zikiwa ni nane nyuma ya FC Barcelona waliokomoa Cadiz 2-0 na kufikisha alama 59 juu ya jedwali. Nao Osasuna wanafunga mduara wa 10-bora kwa pointi 30.

MATOKEO YA LA LIGA (Jumamosi):

Real Betis 2-1 Real Valladolid

Osasuna 0-2 Real Madrid

Real Sociedad 1-1 Celta Vigo

Mallorca 4-2 Villarreal

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Presha kwa Bayern baada ya kichapo kutoka kwa Gladbach...

Pigo kwa PSG baada ya Neymar kupata jeraha dhidi ya Lille...

T L