Na MASHIRIKA
REAL Madrid wanaendelea kuifuatwa Barcelona baada ya kukomoa Osasuna 2-0 ugenini katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumamosi.
Real walikosa huduma za mfumaji Karim Benzema kwenye safu ya mbele katika mchuano huo ulioshuhudia wakifungiwa mabao na Federico Valverde na Marco Asensio.
Mabingwa hao watetezi wa La Liga walipoteza nafasi za kufunga mabao zaidi kupitia kwa Vinicius Jr. Alvaro Rodriguez na David Alaba nao walimtatiza pakubwa kipa Sergio Herrera wa Osasuna.
Baada ya mechi za Jumapili, Real sasa wanakamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali la La Liga kwa alama 51 zikiwa ni nane nyuma ya FC Barcelona waliokomoa Cadiz 2-0 na kufikisha alama 59 juu ya jedwali. Nao Osasuna wanafunga mduara wa 10-bora kwa pointi 30.
MATOKEO YA LA LIGA (Jumamosi):
Real Betis 2-1 Real Valladolid
Osasuna 0-2 Real Madrid
Real Sociedad 1-1 Celta Vigo
Mallorca 4-2 Villarreal
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO