• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Mwigizaji ashtakiwa kwa kushindwa kulipa bili ya Sh152,550

Mwigizaji ashtakiwa kwa kushindwa kulipa bili ya Sh152,550

NA RICHARD MUNGUTI

MWIGIZAJI katika Nairobi Diaries kidosho Diana Clara Ojenge amekana kupokea deni la Sh152,550 katika hoteli moja ya kifahari jijini Nairobi.

Clara alifikishwa mbele ya hakimu mkazi Monicah Morara kwa kula na kunywa katika hoteli ya Golden Ice Bistro iliyoko South C Nairobi.

Mahakama ilifahamishwa Clara alikula kuku Sh3,000, sharubati Sh2,000, chupa mbili za soda Sh500, maji Sh400 na Redbull ya Sh1, 650.

Pia alibugia pombe kali Bellaire Luxe 750ml ya Sh75,000 na Seven Hennessey VS 750ml ya Sh70,000.

Clara alishindwa kulipia maankuli akisema kadi ya Visa ilikua na shida.

Aliomba asindikizwe na wafanyakazi wa hoteli hiyo hadi kwa nyumba kuchukua pesa lakini hakuwa na pesa.

Clara alipelekwa kituo cha polisi cha Akila aliposhtakiwa.

Hakimu alimwachilia kwa dhamana ya Sh50,000 pesa tasilimu hadi Juni 20 kesi itakapotajwa.

  • Tags

You can share this post!

Karua aahidi kuyeyusha umaarufu wa Naibu Rais

UJAUZITO NA UZAZI: Minyoo wanaohangaisha watoto

T L