• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
KASHESHE: Miaka 10 akiwa singo na hajuti

KASHESHE: Miaka 10 akiwa singo na hajuti

NA SINDA MATIKO

MWIGIZAJI Nini Wacera amekuwa singo kwa miaka na mikaka sasa na kisa na sababu ni kwamba mpenzi wake alimchepukia ndani ya wiki moja tu baada yake kusafiri.

Nini anasema alimdeti ex wake Toby kwa miaka mitatu na katika kipindi hicho hakuwa na mashaka na mapenzi yao.

Basi ikatokea safari yake kwenda kushuti filamu kule Nigeria. Kule Nigeria angekaa kwa miezi sita na kutokana na jinsi alivyokuwa ameyaacha mahusiano yao, hakudhani Toby angemchepukia.

“Siku moja nilipata nimepigiwa simu nyingi sana na swahiba wangu kutoka Nairobi na alichotaka kujua ni ikiwa mimi na Toby tumeachana maana alimcheki jamaa yangu na mwelekezi mmoja wa filamu wakiwa kwa mahaba mazito,” Nini kasimulia.

Kilichomuumiza hata zaidi ni kwamba “haikuchukua hata siku 10 toka alipoondoka kabla ya Toby kunichepukia.”

Toka wakati huo aliamua kuwa singo na imepita zaidi ya mwongo mmoja akiwa solo.

  • Tags

You can share this post!

KIKOLEZO: Maisha na mikasa ya nguli Tedd Josiah

KIPWANI: Msupa wa kwanza produza katika Coke Studio ‘19

T L