• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 5:50 AM
Adhabu ya kadi nyekundu dhidi ya David Luiz wa Arsenal yadumishwa,  ya Bednarek wa Southampton yabatilishwa

Adhabu ya kadi nyekundu dhidi ya David Luiz wa Arsenal yadumishwa, ya Bednarek wa Southampton yabatilishwa

Na MASHIRIKA

ARSENAL wamepoteza rufaa ya kubatilisha kadi nyekundu ambayo beki wao David Luiz alionyeshwa wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) iliyowakutanisha na Wolves waliosajili ushindi wa 2-1 ugani Molineux mnamo Februari 3, 2021.

Wakati uo huo, beki Jan Benarek wa Southampton ameondolewa marufuku ambayo vinginevyo ingemshuhudia akikosi jumla ya mechi tatu zijazo za EPL baada ya kulishwa kadi nyekundu kwa kumchezea visivyo fowadi Anthony Martial wakati wa mechi iliyowapa Man-United jukwaa la kuwapokeza kichapo cha mabao 9-0 mnamo Februari 3, 2021.

Katika taarifa yao, Arsenal wamesema wanasikitishwa sana na matokeo ya rufaa yao.

Kwa upande wake, Benarek kwa sasa atakuwa sehemu ya kikosi kitakachotegemewa na Southampton kwenye mechi ijayo dhidi ya Newcastle United mnamo Februari 6, 2021 uwanjani St James’ Park.

Arsenal walikuwa wakijivunia uongozi wa 1-0 katika mchuano huo dhidi ya Southampton kabla ya kufurushwa ugani kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea visivyo Willian Jose da Silva.

Craig Pawson ndiye alikuwa refa wa mchuano huo na maamuzi yake ya kumpa Luiz kadi nyekundu yalidumishwa na teknolojia ya VAR.

Luiz, 33, sasa atakosa mechi itakayowakutanisha na Aston Villa mnamo Februari 6 ugani Villa Park.

Kocha wa Southampton, Ralph Hasenhuttl, amefurahia maamuzi ya kubatilishwa kwa kadi nyekundu ya Bednarek ambaye hakustahili kuadhibiwa kiasi hicho dhidi ya Man-United ugani Old Trafford katika mchuano wao uliopita.

Kikosi hicho kwa sasa kimewaomba vinara wa Shirikisho la Soka la Uingereza (FA) kutoruhusu refa Mike Dean au Lee Mason kusimamia mchuao wao wowote katika siku za baadaye.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Viambajengo muhimu katika lugha kama chombo cha mawasiliano

Buhari ateua mabalozi waliojiuzulu kuwa mabalozi