• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 7:50 AM
Kylian Mbappe aongoza PSG kuzamisha chombo cha Juventus katika UEFA

Kylian Mbappe aongoza PSG kuzamisha chombo cha Juventus katika UEFA

Na MASHIRIKA

KYLIAN Mbappe alipachika wavuni mabao mawili na kusaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kuanza kampeni za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Juventus.

Mbappe aliwafungulia PSG ukurasa wa mabao katika dakika ya tano baada ya kushirikiana vilivyo na Neymar. Bao lake la pili katika dakika ya 22 lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na beki Achraf Hakimi.

Weston McKennie alitokea benchi na kufutia Juventus machozi katika dakika ya 53 baada ya kumzidi ujanja kipa Gianluigi Donnarumma aliyewajibishwa vilivyo na Dusan Vlahovic katika vipindi vyote viwili vya mchezo.

Neymar alipoteza nafasi nyingi za kufungia PSG bao la tatu licha ya kusalia peke yake na kipa Mattia Perin aliyepangua na kudhibiti makombora kadhaa aliyoelekezewa na kigogo Lionel Messi.

Benfica kutoka Ureno ilipepeta Maccabi Haifa ya Israel 2-0 katika pambano jingine la Kundi H.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Uhuru bado kuamini Ruto alishinda urais

TAHARIRI: Serikali inayoingia isipuuze matatizo ya afya ya...

T L