• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 7:55 PM
Masikitiko Gor ikibanduliwa Caf nyumbani

Masikitiko Gor ikibanduliwa Caf nyumbani

Na CECIL ODONGO?

VIGOGO wa soka nchini Gor Mahia jana walibanduliwa kwenye kipute cha Kombe la Mashirikisho Afrika (CAF) baada ya kuandikisha sare ya 1-1 dhidi ya AS Otoho d’Oyo ya Jamuhuri ya Demokrasia ya Congo kwenye mechi ya raundi ya pili uga wa Kitaifa wa Nyayo.

Gor ilibanduliwa kwa jumla ya 2-1 kwa kuwa AS Otoho ilishinda mechi ya mkondo 1-0 jijini Brazzaville wiki jana.Mvamizi Roland Okouri ambaye alifunga bao kwenye mkondo wa kwanza alizamisha Gor baada ya kuweka AS Otoho d’Oyo mbele kipindi cha kwanza dakika ya 12.

Hata hivyo, K’Ogalo ilijituma na kupata bao dakika mbili baadaye kupitia John Macharia.?Okouri alifunga baada ya kichwa cha Chandrel Massanga kugonga mlingoti kutokana na mpira wa ikabu uliochanjwa na Fariah Ondongo nje ya eneo hatari.

Naye Macharia alijaza mpira wavuni baada ya kipa Wilfrigon Mongondza kupangua krosi ya Fred Nkata.Huu ni mwaka wa tatu mfululizo ambapo Gor imekosa kutinga hatua ya makundi ambayo huja na kitita cha Sh27 milioni kutoka Caf.

Matokeo hayo yalikuwa pigo kwa maelfu ya mashabiki wa Gor waliofurika ugani Nyayo kwa mechi.Msimu uliopita K’Ogalo ilibanduliwa na Napsa Stars ya Zambia kisha msimu uliotangulia walilemewa na DC Motema Pembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

AS Otoho sasa wametinga hatua ya makundi baada ya kulemewa 4-2 na Petro de Luanda ya Angola katika raundi ya kwanza ya Klabu Bingwa Afrika (CAF).Gor nao walifuzu raundi ya pili baada ya kuilemea Al Ahly Merowe ya Sudan 3-1 katika raundi ya kwanza.

Wawakilishi wengine Wakenya Tusker jana iliratibiwa kuchuana na CS Sfaxien nchini Tunisia baadaye jana jioni.Kocha wa Gor Mark Harrison alisikitikia kichapo hicho akisema kuwa vijana wake walifanya makosa ya kijinga.

‘Nimetamauka na matokeo haya. Ingawa tulikuwa na wachezaji 16 pekee, baadhi ya makosa yaliyofanyika ni ya kijinga na yangeepukika,’ akasema Harrison.’Inasikitisha tumebanduliwa lakini sasa hatuna jingine ila kumakinikia ligi.

Ni uchungu sana kung’atuka Caf,’ akaongeza.Mwenzake Alou Badra alisifu vijana wake, akisema walicheza kana kwamba walikuwa nyumbani.’Tumefuzu na licha ya kuwa ugenini, tulifunga na kupoteza nafasi kadhaa. Heko kwa timu yangu na sasa tutalenga maandalizi ya mechi za makundi ‘ akasema Badra.

You can share this post!

Arsenal kwenye mizani

Wakenya Nancy Cherono, Jelagat wavuna vinono Valencia...

T L